FOLLOWERS

Friday, October 28, 2011

SIMBA VS YANGA, KIVUMBI KESHO

 Wachezaji wa timu ya Simba wakiomba dua katika moja ya mechi za na watani wao wa jadi Yanga


 Wachezaji wa timu ya Yanga wakiomba dua katika moja ya mechi za na watani wao Simba


          Kikosi kamili cha wakali wa msimbazi, Simba Sports Club ya jijini Dar-es-salaam


Kikosi kamili cha wakali wa mtaa wa jangwani, Dar Young African (Yanga) ya jijini Dar-es-salaam.

Macho na masikio ya mashabiki wote wa soka Tanzania kesho yataelekezwa katika uwanja wa taifa ambapo watani wa jadi Simba na Yanga watakuwa wakikpepetana katika mchezo wa mzunguko wa kwanza wa ligi kuu soka ya vodacom Tanzania bara. Simba wataingia uwanjani wakiwa na kumbukumbu nzuri ya kuwatandika watani wao hao mabao mawili kwa sifuri (2-0) katika mechi ya ngao ya hisani ambayo ilikuwa ni ishara ya kufungua msimu mpya wa ligi hiyo..papo hapo Yanga wao wataingia na matumaini wakiwa na kocha wao mpya PAPIC baada ya kimtimua kocha wa awali SAM TIMBE na wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao moja kwa sifuri katika mechi yao iliyopita huku Simba wao wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa mabao mawili kwa sifuri katika mechi yao iliyopita ya ligi….Dakika 90 zitakazosimamiwa na mwamuzi OdenMbaga hapo kesho ndizo ziatakazoamua nani ni nani kati ya Simba na Yanga….YETU MACHO

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...