FOLLOWERS

Wednesday, July 11, 2012

SIMULIZI : WAZIRI WA MAMBO YOTE SEHEMU YA 01

Na Fredy Julius


UTANGULIZI
Naomba nianze kwa kusema kuwa, binadamu hawezi kuwepo bila ya mazingira kwa sababu binadamu anategemea mazingira, mazingira yanaweza kuendelea kuwepo na kustawi kwa miaka mingi ijayo kwa sababu mazingira hayamtegemei binadamu. Binadamu anapoharibu mazingira anajiharibia nafasi ya kuendelea kuwepo katika mazingira husika. Sasa basi kama sisi binadamu tunatamani na tunataka kuendelea kuonekana katika uso wa hii dunia ni lazima na hatuna budi kuhakikisha kuwa tunatumia nguvu zetu nyingi katika kutunza, kuhifadhi na kuendeleza ubora wa mazingira haya kwa sababu bila ya kufanya hivyo maana yake ni kwamba tunatengeza mazingira ya mahangaiko yetu wenyewe na hatimaye kufutika kabisa katika uso wa hii dunia. Moja ya mambo ambayo yanaathiri maish ya binadamu kwa kiwangi kikubwa ni uharibifu wa mazingira n akwa sababu asilimia kubwa ya wananchi hawajui umhimu na uhusiano iliopo kati ya binadamu na mazingira hawaioni hatari ambayo ipo karibu yetu kutokana na kuharibu mazingira yanayotuzunguka. Kitu amabcho ni hatari kwa maisha yetu na ya vizazi vyetu vijavyo…………..SASA ENDELEA.

           
Hivi Chriss ni kwanini hawa ndugu zako wapo hivi, mbona mambo wanayoyafanya ni tofauti kabisa na jinsi ambavyo wewe umekuwa ukiwafanyia?. Hivi huyu si yule shangazi yako ambaye mwanae ulimsaidia kumfundisha mpaka akafaulu vizuri kidato cha sita lakini yeye anakudharau kama vile huna mchango wowote katika maisha yake halafu na wewe unaona ni sawa tu? Wala hupotezi muda wako kujiuliza ni kwanini na ikibidi uwe unawaambia ukweli, mimi naona wanavyokutendea sio sawa kabisa inabidi angalau wakuheshimu na kujali na kuthamini mchango ambao tayari umeshatoa katika maisha yao. Kwa sababu hata yule baba yako mdogo naye tabia zake sio nzuri. Ameamua kukudhulumu kiasi kikubwa kabisa cha pesa lakini wewe hata hujali, hivi ni kwanini uko hivyo wewe?
Hivi unanisikiliza ninyoyaongea au uko mbali na hapa tulipo, maana naona hujibu kitu, akaamua kuuliza Ephraim baada ya kuona rafiki yake yuko mbali kimawazo na ni kama hamsikilizai maneneo anayoyaongea. “ nakusikiliza sana na nakuelewa unayoyaongea, sema mawazo yangu yametekwa na kipindi kijacho cha bunge naona kama tutachelewa kutazama nataka nijue ni mswaada gain utaletwa leo na nini kauli za mheshimiwa wetu waziri wa mambo yote, ujue huwa simuelewi kabisa kiasi nashindwa nimuweke upande gain, ni mzalendo kwelei au ni mnafiki tu nay eye ni mmoja ya watu wanotafuna rasilimali za nchi hii bila kutazama jinsi wazee wetu wanavyopata taabu huko vijijin”?. Sikiliza nikwambie rafiki yangu, hawa ndugu zangu mimi nimeshawazoea sana na wala hwanipi tabu na nimeshamua na kukubali kuwa wao ni wao na mimi ni mimi na kwa kawaida sipendi kujiuliza kwanini sijalipwa fadhila za mema yangu ambayo nimeyatenda kwa mtu yeyote kwa sababu naamini wao sio mimi kiasi watambue malipo ya wema.
Sasa nisikilize, wakati tunaendelea kuzungumza naona ni vizuri tukaongeza mwendo ili tusichelewe kipindi cha bunge cha jioni maana ni hamu sana na maneno ya wabunge juu ya huu muswaada uliowasilishwa, yaani kuna wengine wanautetea kana kwamba hawaoni kuwa wanafuta maandishi ya wino wanaadnika kwa kalamu ya risasi, halafu labda leo na mbunge anayewakilisha jimbo letu naye anaweza kuongea watu tukamsikia maana tangu aende huko bungeni hajawahi kuongea chochote na kama amewahi kuongea basi ni siku ambayo mimi sikutazama televisheni au unasemaje? Kweli, rafiki yangu lakini mbona unamuita mbunge anayewakilisha jimbo letu kwani wewe siyo mbunge wako? Kwanini usiseme mbunge wetu? Waapi siwezi kusema mbunge wangu akati sikumpigia kura na wala hakuna mwananchi ktoka katika jimbo letu ambaye alipiga kura ya kumchagua mbunge, alipigiwa kura na watu wa chama chake akapitishwa sasa we unadhani anamuwakilishaje mwamanchi ambaye hakumchagua? Yule yupo kule kuwakilisha jimbo letu wala sio kuwakilisha wananchi maana hata mara moja sijawahi kusikia kuwa amekuja kufanya mkutano na wananchi.
 Haya kaka, tuyaache hayo, rakini hata mimi nawasikia wananchi weengi tiu wanalalamika juu ya huyu mbunge wa jimbo letu kuwa wamemchoka hata miaka mitatu haijaisha, hivi kwanini tusifanye utaratibu wa wananchi kumbadilisha mbunge na wamchague mwingine ambae wao wanahisi atawafaa? Hilo ni sawa ila labda katika katiba hiyo mpya inayokuja maana hata kwa uelewa wangu mdogo kuhusu sheria mbunge hawezi kubadilishwa na wananchi hata kama wananchi wao ndo wamempigia kura labda mpka mwenyeew aamue kujiuzulu au chama chake kimfute uanachama maana katika katiba ya sasa hakuna kipengele kianchoelezea kuwa wananchi wananweza kumuondoa mbunge katika nafasi yake. Haya ya kuhusu ukomo wa mbunge kushika nafasi yake katika katiba ya sasa yameelezwa katika ibara 71 kifungu cha kwanza kama ifuatavyo; 71 (1) mbunge atakoma kuwa mbunge na ataacha kiti chake katika bunge litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo; (a) ikiwa litatokea jambo lolote amabalo, kama asingekuwa mbunge lingemfanya asiwe na sifa za uchaguzi au apoteza sifa za uchaguzi au asiweze kuchaguliwa na kuteuliwa kwa mujibu wa masharti ya katiba hii. (b)Ikiwa mbunge huyo atachaguliwa kuwa raisi (c) Ikiwa mbunge atakosa kuhudhuria vikao vya mikuatano ya bunge mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya spika. (d) Ikiwa itathibitishwa kuwa amevunja masharti ya sheria ya viongozi wa umma. (e) Iwapo mbunge anachaguliwa au anateuliwa kuwa makam wa raisi (f)Iwapo mbunge ataacha kuwa mwanachama wa chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au alipoteuliwa kuwa mbunge (g) Kwa mbunge ambaye anatakiwa kutoa taarifa rasmi ya mali kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 70, ikiwa atashindwa kutoa hilo tamko rasmi kwa mujibu wa masharti ya hiyo ibara ya 70 katika muda uliowekwa mahususi kwa ajili hiyo kwa mijibu wa sheria iliyotungwa na bunge,                                                                                                                                  lakini iwapo mbunge hatakoma kuwa mbunge kwa mujibu wa jambo lolote kati ya mambo hayo yaliyotajwa na kama hatajiuzulu au kufariki mapema zaidi basi mbunge ataendelea kushika madaraka yake kama mbunge mpaka wakati bunge litakapovunjwa kwa mujibu wa ibara ya 90, bila kuathiri haki na stahili zizotoka na ubunge wake.
Sasa Ephraim hembu niambie, kwa mujibu wa katiba jinsi ilivyo, we unadahini mbunge anawajibika kwa wanacnhi kweli au anawajibika kwa chama chake ambacho ndio kimempa nafasi ya kugombea na kuwa mbunge? Haya achana na hao wabunge ambao wamechaguliwa na wananchi angalau kidogo wanaona haya hata kwa maneno na lawama za wananchi kila kukicha juu ya ugumu wa maisha. Hivi kwa mbuge anayewakilisha jimbo letu, kweli kabisa atawajibika kwa wananchi ambao hata kumachagua hawakumchagu na hawana mamlka kwa mujibu wa katika ya kumuwajibisha, au atawajibika kwa chama chake hiki cha mageuzi amabcho ndio kilichomteua na kupelekea yeye kuwa madarakani kwa kupita bila ya kupingwa, yaani hata kumpigia kura ya kuwa au ktukuwa na imani naye ili kumthibitisha kuwa ndio mbunge wa wanachi wa jimbo hili hamna halafu tunataka awajibike kwa wananchi, kweli inawezekana?.hapana.
Chriss hapo hata mimi naona kama mbunge sio wetu bali ni wa chama ambacho ndio kimempa madaraka na kina uwezo wa kumnyang’anya madaraka hayo, hapo kwa vyovyote ni lazima mbunge awajibike kwa chama chake, hiyo iko wazi. Sasa umeona? Achana na huyu wa jimbo letu, je hawa wa kuteuliwa watawajibika kwa nani ikiwa hawachaguliwi na wananchi? Kwa vyovyote vile ni lazima watawajibika kwa chama chao na ndiuo maana utawaona wabunge wa kuteuliwa wa chama tawala wanashabikia sera na mipango amabayo haina mantiki wa tija kwa maendeleo ya taifa hili hata kidogo, maswali ya msingi nay a nyongeza wanayoyauliza hayaeleweki na wanaongoza kwa kuwasifia mawaziri, utasikia “ namshukuru sana muheshimiwa waziri kwa majibu mazuri na yenye kuleta tija, na kwa kuwa naamini serikali ya chama changu ni sikivu basi naamini haya yatatendewa kazi, lakini hata hivy muheshimiwa spika nina swali dogo moja la nyongeza, kwa kuwa ni tangu mwaka juzi serikali imewaahidi wanachi wa mkoa wangu kuwa misaada na mikopo kwa akina mama na wajasiliamali wadogowadogo itafikishwa moja kwa moja kwa wahusika, na kwa kuwa wahusika wanalalamika kila siku kuwa mpaka leo hawajapata hayo mabilioni tangu yalipotolewa, sasa je, ni lini mheshimiwa wazri atawawajibisha watendaji wake na kuwaagiza kuwa wahakikishe wanapeleka pesa hizo moja kwa moja kwa wananchi badala ya kupitishia katika mtirirIko huo ambao unasababisha ubabaishaji mwingi na hatimaye wanachi wengi wa hali ya chini kuzikosa pesa hizo”?. Sasa hapa utajiuliza uhalali wa kusifia majibu yaliyotolewa na waziri pamoja na kuuliza swali la nyongeza kama hilo……………….ITAENDLEA WIKI IJAYO
MAONI, 0766948187
 


No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...