FOLLOWERS

Thursday, August 23, 2012

SAKATA LA BAADHI YA WAISLAMU NA SENSA BADO UTATA

Sensa ni muhimu kwa nchi yoyote kwa maana kwamba ni sherti serikali ijue idadi ya watu wake na mahali wanapoishi.

Takwimu na taarifa hizo ndio msingi wa upangaji wa mipango yoyote ya huduma na maendeleo. Kwa akili yangu finyu, huu ni ukweli usiopingika.


Kama kuna sehemu ambapo watu hawajahesabiwa, sehemu hiyo itaonekana iko wazi; haina watu. Kwa maana hiyo, hakutakuwa na msingi wowote wa kuiingiza sehemu hiyo katika mpango wa huduma au maendeleo.


Sehemu itakayoonekana haina watu itawekwa kando katika mipango hiyo ya huduma na maendeleo. Sasa basi, endapo kulikuwa na watu sehemu hiyo, ambao walisusia sensa, wasije wakajitokeza baadaye na kulalamika kuwa wanaonewa.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...