FOLLOWERS

Thursday, August 2, 2012

MAMBO YA TEHEMA UDOM

Katika kuhakikisha kuwa tunakwenda na kasi ya teknologia inayoenda kwa kasi duniani, Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) sasa kimeanza rasmi kufundisha kwa kutumia mtandao na kuhakikisha kila mhadhiri, anafundisha madenti wengi kwa wakati mmoja.
Hilo liliwekwa wazi juzi na Balozi Juma Mwapachu, alipokuwa akizungumza na wahadhiri wa Udom katika ufunguzi wa mafunzo ya ufundishaji kwa njia ya teknolojia hiyo.
Mwapachu ambaye pia ni Mwenyekiti wa baraza la chuo hicho, alisema wingi wa wanafunzi katika chuo hicho kikubwa kwa sasa hauendani na idadi ya wahadhiri waliopo na kwamba bila ya kuwa na mbinu mbadala za kuwafundisha, wanafunzi wataachwa nyuma.
“Udom sio chuo cha kawaida katika nchi za Afrika Mashariki, lakini pia niseme kuwa siyo vyuo vingi hapa duniani vimeweza kupata bahati ya kukua kwa kasi kubwa ndani ya miaka minne kama Udom, kwa hiyo ukuaji wa chuo hiki lazima uwe wa kisasa na unaokwenda na sayansi na teknolijia,” alisema
Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Udom, Prof Idris Kikula, alisema chuo kilikuwa kinakabiliwa na tatizo katika ufundishaji, hatua iliyoulazimisha uongozi kubuni mkakati huo.Kikula alisema hatua ya sasa ni ya kuwajengea uwezo wahadhiri, ili waweze kufanyakazi zao kwa ufanisi mkubwa zaidi.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...